“Nimezungumzia mapenzi kwa upande wa mwanamke kuzungumzia mwanaume japo ni wimbo ambao unaweza kutumika kwa pande zote mbili, nimebeba uhusika wa mwanamke kwa mimi ni mwanamke pia” amesema Nandy.
“Ni maumivu ya mapenzi mwanamke analalamika kwa wanaume wake kuna kitu amemfanyia lakini so far anahitaji amuache kwa sababu anaamini taratibu maamuivu yake yataisha taratibu” ameongeza.
Nandy ambaye bado anafanya vizuri na ngoma ‘Wasikudanganye’, pia hivi karibu alitoa ngoma iliyokwenda kwa jina Mahabuba ambayo amemshirikisha Aslay.
0 comments:
Post a Comment