Friday, 7 July 2017

Alikiba", Baraka The Prince Bado anaakili za kitoto.

Hit maker wangoma ya Aje amesema hayo baada ya kuulizwa kwamba kwa sasa hawaonekani kuwa karibu na Baraka kama zamani huku tetesi zikidai kwamba ukaribu wao umevunjika baada ya Alikiba kuwa karibu na Ommy Dimpoz.


Alikiba alisema  “Mimi nadhani ni utoto tu, nadhani ni umri tu lakini Baraka yupo vizuri, ni mtu anayesikiliza na ana rekebishika. Muda mwingine labda umri ndio unampeleka lakini muda mwingine mtoto akifanya jambo unamwambia,” Alikiba alikiambia kipindi cha XXL cha Clouds FM. “Ni mdogo wetu tutamwelimisha na sidhani kama anamchukia Ommy Dimpoz labda ni maneno tu ya mtaani,”
.
Na Kwa upande wa Ommy Dimpoz ambaye alitambulisha wimbo wake mpya Cheche, amedai yeye hajawahi kugombana na Baraka na wala hana tatizo na mtu yeyote.

1 comment:

  1. Braka bado anawenge la ustar ila atakuwabado mdtoto kweli uyo

    ReplyDelete

Copyright © MOtown TV | Designed With By Blogger Templates
Scroll To Top