Rapa Young Killer Msodoki.
Young Killer amebainisha hayo baada ya kuwepo dimbwi kubwa la mashabiki kufuatilia na kuchimbua maisha binafsi ya wasanii na kuwaanika katika mitandao mbalimbali ya kijamii jambo ambalo limepelekea watu kupenda 'udaku' zaidi kuliko hata kujua ni kazi gani mpya ya msanii ameitoa au anaifanya kwa kipindi hiki.
"Now days watu wamekuwa wanapenda vitu vya hovyo sana yaani vile vitu 'real' ambavyo vinafanya sisi tuwe katika nafasi ambayo tulikuwepo vinakuwa vinapotezwa na vitu vya 'kipumbavu' sana", amesema Youngkiller.
Pamoja na hayo, Young Killer ameendelea kwa kusema "mitandao imekuwa mingi, maisha yetu yote sasa hivi watu wanatuchukulia poa tu, so hiyo nadhani inachangia kushusha hata 'mode' ya kufanya kazi nzuri". Alisema Youngkiller

0 comments:
Post a Comment